Thursday, June 9, 2011

KARIBU KATIKA USHARIKA WA KIMARA KWA HUDUMA YA IBADA YA MAOMBEZI KWANI WENYE SHIDA MBALIMBALI WATAOMBEWA

HAPA MPAKA KIELEWEKE!!

Mtumishi wa Mungu kutoka Uganda Steven Katto akichemka bila ya kifuniko katika mkutano ulofanyika kimara hivi karibuni
Mmoja kati ya waumini walowahi kuhudruria ibada za katikati ya wiki wakitoa shuhuda zao mbalimbali ambazo mungu amewatendea mara baada ya maombezi

NAO WALIOKUWA NA SHIDA MBALIMBALI WALIFANYIWA MAOMBI!!

Mtumishi Mercy akiwa katika moja kati ya huduma ya maombezi

SEHEMU YA WATU KATIKA MKUTANO HUO!!!

VIPI HAPO UMEONAEE!!!!


Kaka hongera sanaaaaaaaaaaaaa

KATIKA WIKI YA KWANZA YA MKUTANO NAYE HUYU ALIAMUA KUACHANA NA MAISHA YA UKAPERA!


Mtumishi wa Mungu David Ongollo nae aliamua kuachana na maisha ya ukapera na kuamua kufunga ndoa katika kanisa la Kimara huwezi kuamini yaaaaani walitia fora mbaaaaaaaya
Umati huu wa watu uliamua kusimama na mkutano huo kwa njia ya matoleo hapa ni baada ya mahubiri kwa kweli kupitia mkutano huu MUNGU alijidhihirisha.
Kwa kwel ilikuwa ni ngumu kumtambua lakini kama nilivyo kwambia ngoma ilikuwa ikichemka bila ya kifuniko mpaka mida ya usiku na hapa ni mtumishi mpakwa mafuta kutoka Uganda Steven Katto akichemuka bila ya kifuniko.

JIONEE MWENYEWE

Hii ni baadhi ya sehemu ya viti ambavyo vilitumika katika mkutano huo na hapa ni kabla ya mkutano kuanza kwa kweli jina la Bwana wetu Yesu Kristo mahali hapa lilitukuka.

HII NDIO KIMARA BWANA!!

Hivi karibuni usharika wa Kimara uliandaa mkutano mkubwa wa Injili ambao ulifanikiwa kukusanya watu kutoka maeneo mbalimbali na watu wengi kwa kweli walifunguliwa kupitia Mkutano huo ambao wahubiri walikuwa ni Steven Katto na Godfrey Waswa wanaofahanika zaidi kama MAPACHA kutoka Uganda.
   Kutokana na muamko wa Injili kwa sasa licha ya mahubiri kuchelewa kuanza hii ni kutokana na miundombinu ya jiji letu lakini bado watu walionekana kumudu mpaka mida ya saa tatu usiku.
Kama kawaida yako Blog hii inakuletea yale yote yalojiri katika mkutano huo.